Flickr Photos

Gallery

VITA KATI YA BABA NA MAMA KANUMBA PABAYA....matusi njenje

BABA wa aliyekuwa msanii maarufu wa filamu Bongo, marehemu Steven Kanumba, Charles Kanumba ameibuka na kumtaka mama Kanumba, Flora Mtegoa kuacha tabia ya kuombaomba michango mbalimbali.
Baba wa aliyekuwa msanii maarufu wa filamu Bongo, marehemu Steven Kanumba, Charles Kanumba.
Akipiga stori na paparazi wetu, Baba Kanumba alisema anashangazwa na tabia ya mama Kanumba kuombaomba ambapo hivi karibuni alimuona mjini Shinyanga ambako alikuwa akiomba rambirambi kwenye kumbi za starehe.
“Namshangaa mama Kanumba ni njaa gani hiyo, naomba aache kudhalilisha ukoo wa Kanumba kwani anatumia jina hilo kuombaomba, anahangaika bila sababu za msingi wakati sisi tuko vizuri,” alisema Baba Kanumba.
Mama Kanumba, Flora Mtegoa.
Akijibu tuhuma hizo, mama Kanumba alisema kama ana malalamiko yoyote aende mahakamani maana yeye si mume wake. “Aache kunifuatafuata kwani mimi si mkewe na Shinyanga nilialikwa kwenye Miss Shinyanga siyo kwamba nilijiendea tu,” alisema.
0 Komentar untuk "VITA KATI YA BABA NA MAMA KANUMBA PABAYA....matusi njenje"

Back To Top