Flickr Photos

Gallery

RIHANNA AKAA MEZANI NA DROGBA KUJADILI TIMU GANI AINUNUE


Rihanna anasemekana kuwa na nia ya dhati kutaka kununua club ya soka ya Uingereza na tayari amezungumza na Didier Drogba ambaye ni rafiki yake wa karibu ili ampe ushauri.

Muimbaji huyo mwenye miaka 26 pia amepanga kuanzisha chuo cha michezo nchini kwao Barbados na kisha anapenda kuwa mwenyekiti ama mmiliki wa club kubwa ya Uingereza. 

Chanzo kilicho karibu na Rihanna kilidai kuwa awali alidhani muimbaji huyo alikuwa akitania tu kuhusiana na jambo hilo lakini amegundua kuwa yupo serious
 
Rihanna ni shabiki wa Liverpool. Katika kombe la dunia lililomalizika nchini Brazil, Rihanna alikuwa shabiki mkubwa wa timu mbalimbali zikiwemo Brazil na Ujerumani.
Tag : cate-michezo
0 Komentar untuk "RIHANNA AKAA MEZANI NA DROGBA KUJADILI TIMU GANI AINUNUE"

Back To Top